Sunday 23 December 2012

GUSAGUSA MINIBAND KUZINDUA 'UNAJIDODO LINAKUCHUKUCHA' MWAKA WA 2013.....

 
Bendi la Gusagusa Miniband linapanga kuzindua rasmi album yao ya kwanza kwa jina la 'Unajidodo Linakuchukucha' mwaka huu wa 2013 baada ya kukamilisha album hiyo.

Kulingana na mmoja wa wawakilishi wa kundi hilo Foni Chupaa, Album hiyo itazinduliwa rasmi mwezi ujao (Februari) na itakuwa na jumla ya vibao vinne ndani ikiwemo kibao cha 'Unajidodo linakuchukucha by Afua Suleiman, Mapenzi hayana Formula by Swabaha Salum, Usishindane na alojaaliwa by Maryam Alawy na Azurure atachoka/Inawaumaje by Ally Hassan.

"Tumeona uzinduzi kila mtu anazindua, tarehe yetu tumesogeza mbele kwa maoni na washabiki wa gsgs, na utakuwa uzinduzi babu kubwa kwa mara ya kwanza kwa hiyo matarajio yetu mwezi wa pili, lakini tutawatangazia rasmi tarehe ngapi na siku gani, na siku hiyo albam ya unajidodo itauzwa na kuanza kuwa maduka rasm." Anasema Foni Chupaa.

"MAMBO SHWARI KATI YANGU NA DADANGU" - MZEE YUSSUF....

Mfalme Mzee Yussuf amepinga vikali kuwa uhusiano kati yake na dadake Khadija Yussuf umekumbwa na mushkil kwa mara nyengine tena.

Akizungumza na Blogu hii moja kwa moja, Mzee amekiri kuwa uhusiano kati yake na dadake Bi. Khadija Yussuf uko imara wala hautawahi kuvunjika.

“Uhusiano kati yangu na dadangu bado uko imara wala hautawahi kuvunjika kama wanavyotaka wapambe,” Anasema Mzee Yussuf.

Haya yanajiiri baada ya Bi. Khadija Yussuf kupitia kipindi cha ‘Sham Sham za Pwani’ kinachorushwa kupitia runinga ya ITV kuangua kilio akidai kuna ‘Vidudu watu’ ndani ya bendi la jahazi wanaopeleka maneno ya urongo kwa kaka yake ili kuwagombanisha kiasi cha kuwafanya wasielewane vizuri.

"Kinachoniuma zaidi ni kwamba afadhali hayo maneno ningekuwa nimeyasema, lakini sijafanya hivyo, Hawa watu wanapaswa kutambua kwamba kuna Mungu na mimi na Mzee Yussuf tumezaliwa baba mmoja mama mmoja, atakapozikwa Mzee Yussuf ndipo nitakapozikwa mimi,"alisema Khadija huku machozi yakianza kumlengalenga.
 

"Kusema kweli maisha ninayoishi na Mzee Yussuf hivi sasa ni tofauti na huko nyuma tulikotoka, Inaniuma sana,"alisema Khadija na kuangua kilio kikali.

Mapema Khadija alisema kuna kikundi cha watu ndani ya Jahazi, ambacho kimekuwa kikimchonganisha yeye na wifi yake, Leila Rashid, ambaye ni mke wa pili wa Mzee.


Alisema watu hao wamekuwa wakipeleka maneno ya umbeya kwa Leila wakidai kuwa yeye ndiye ameyasema na vivyo hivyo wamekuwa wakija kwake na kumweleza maneno kama hayo.
 

"Kuna wakati Leila amekuwa akinitumia meseji zenye maneno machafu, Ninapomjibu anakasirika,  Sielewi tunachogombea ni kipi,"alisema Khadija.
 

"Binafsi sina tatizo na Leila na sioni kwa nini tugombane, Sielewi na ninashangaa, Lakini hii yote ni kwa sababu kuna watu ndani ya Jahazi wanaotuchonganisha kwa makusudi,"aliongeza.
 

Hata hivyo juhudi zetu za kumtafuta Malkia Leila Rashid zinaendelea kwa sasa ili tubaini yanayoendelea kati ya wawili hao.


MZEE YUSSUF AMTOLEA MBAVUNI AMIN SALMIN...

MKURUGENZI wa Jahazi Modern Taarab, Mzee Yussuf amesema wataikaribisha bendi yoyote kwenye uzinduzi wa albam yao lakini kamwe si T-Moto Modern Taarab ya Amin Salmin.

Mzee Yussuf ameimabia Saluti5 kuwa kamwe hatapiga jukwaa moja na bendi hiyo kwa vile amegundua kuwa bendi hiyo imejaa ushindani wa chuki badala ya ushindani wa maendeleo.

Jahazi wanatarajiwa kuzindua albam yao mpya “Wasi wasi wako” Jumapili ya tarehe 30 mwezi huu katika ukumbi wa Travertine Hotel, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Kwa muda mrefu Mzee Yussuf na Amin Salmin wameripotiwa kuwa na bifu zito na hata bendi zao zilipokutana kwenye tamasha la Mitikisiko ya pwani mwezi uliopita kwenye ukumbi wa Dar Live, hali ya hewa ilichafuka na wawili hao walikaribia kutupiana makonde.

“Siwezi kupanda jukwaa moja na T-Moto, ni bendi changa inayotaka kupanda juu kwa kutumia mgongo wetu, watafute njia nyingine” alisema Mzee Yussuf na kuongeza kuwa bendi nyingine yoyote ya taarab itakayojiskia kupanda jukwaa la Jahazi siku ya uzinduzi wao, inakaribishwa sana."

Huku hayo yakijiri....Wakaazi wa mji wa Morogoro wanausubiri ujio wa kundi la Jahazi Modern Taarab kwa hamu kubwa ambapo tayari onyesho la bendi hiyo limekuwa gumzo la kila kona ya mji huo.

Jahazi Modern Taarab wanatarajiwa kufanya onyesho kubwa ndani ya ukumbi wa Savoy Hotel siku ya mkesha wa X-Mas Jumatatu 25/12/2012.

Onyesho hilo ni maalum kwa ajili ya utambulisho wa nyimbo mpya kabisa zinazounda albam mpya ya “Wasi wasi wako” yenye jumla ya nyimbo sita.

Courtesy of Salut5 


ISHA MASHAUZI AKIRI YUPO KWENYE MAHUSIANO ILA NDOA BADO SANA....

MKURUGENZI wa kundi la Mashauzi Classic, Isha Mashauzi, amekiri kuwa baada ya kuachana na mumewe, sasa hivi yupo kwenye mahusiano mapya na mwanaume mwingine.

Akiongea kwenye kipindi cha Tagz Weekly cha DTV hivi karibuni, Isha alisema anaye mpenzi mpya ambaye anampenda sana, wanasaidiana na kusikilizana.

Alipoulizwa kuhusu ndoa, Isha alisema ndoa inapangwa na Mungu, ila kwasasa bado sana.

Courtesy of Salut5

Wednesday 19 December 2012

KIBAO CHA 'WASIWASI WAKO NDIO MARADHI YAKO' CHAMTOA KIJASHO MZEE YUSSUF....

Hivi karibuni, Mfalme wa taarab, Mzee Yussuf alikuwa na kibarua kigumu wakati wa kurekodi wimbo wake mpya na kulazimika kuomba mapumziko kila dakika.

Wimbo huo “Wasiwasi wako” ambao utabeba jina la albam mpya itakayozinduliwa tarehe 30 mwezi huu, ulimpa shida Mzee Yussuf kutokana na jinsi ulivyo na njia nyingi za kupanda na kushuka na kumfanya Mfalme huyo wa taarab atumie nguvu nyingi za kusukuma sauti.

Mara kadhaa Saluti5 (mtandao wa burudani) ilimshuhudia Mzee akilazimika kukaa chini na kuugulia koo lake na kama si ukali wa Producer Bakunde, basi kazi hiyo ingeahirishwa kwa mara nyingine tena. 

Nyimbo 5 kati ya 6 zitakazounda albam hiyo zilishakamilika tangu wiki iliyopita, lakini Mzee Yussuf amekuwa mgumu wa kumalizia wimbo wake ambapo kila wakati alikuwa akiibuka na sababu kadhaa zikiwemo malaria na mafua. 

Hivi karibuni, Mzee alisema amefunga ‘sunna’ na ingemuwia vigumu kurekodi wimbo huo, lakini Bakunde alimwambia kwa jinsi ratiba yake ilivyo hapo studio, kama wangeshindwa kurekodi juzi basi ingemlazimu kuifanya kazi hiyo baada ya uzinduzi wa albam jambo ambalo lingekuwa halina maana kwa sababu Jahazi wanataka kuuza CD za nyimbo mpya siku ya uzinduzi.

Kutokana na hali hiyo, Mzee hakuwa na namna nyingine zaidi ya kuingia studio na kurekodi wimbo wake, kazi ambayo ilijaa vituko, malalamiko na usumbufu mwingi kutoka kwa mkurugenzi huyo wa Jahazi.

“Wasi wasi wako” ni kazi nyingine itakayodhihirisha ubora wa Mzee Yussuf ambapo mbali na vionjo vya kuvutia, utakutana na ngoma za sindimba ndani yake hali itakayokufanya ushuhudie mapinduzi mengine ndani ya muziki wa taarab.

Nyimbo zingine zinazounda albam hiyo itakayozinduliwa katika ukumbi wa Travertine, Dar es Salaam ni pamoja na Mambo Bado (Khadija Yussuf), Kazi Mnayo (Mohamed Ali Mtoto pori), Nipe Stara (Rahma Machupa), Hata bado Hujanuna (Fatma Ali Mama Shughuli) na Sitaki Shari (Leila Rashid). 

Wakati huo huo kundi la Jahazi Modern Taarab linatarajiwa kufanya onyesho kubwa mjini Morogoro siku ya Mkesha wa X-Mas.

Mkurugenzi wa kundi hilo, Mfalme Mzee Yussuf, ameiambia Saluti5 (Mtandao wa burudani) kuwa onyesho hilo litakuwa ni mahsusi kwa ajili ya kuupima uzinduzi wao utakaofanyika jijini Dar es Salaam Disemba 31.

Onyesho la Morogoro litakuwa kama ndio ‘Listening Party’ yetu, tutapiga nyimbo zote za albam mpya na kuangalia namna zitakavyopokewa na mashabiki wa Moro na kisha baada ya hapo tutajua nini cha kupunguza au kuongeza kwenye onyesho letu la uzinduzi" alifafanua Mzee Yussuf. 

Wakazi wa Morogoro watashuhudia onyesho hilo siku ya Jumatatu ya tarehe 24 ndani ya ukumbi wa Savoy Hotel.

Na huku hayo yakijiri...Mwimbaji wa Jahazi Modern Taraab, Monica Robert, maarufu zaidi kama Mwasiti, anatarajiwa kufunga ndoa na mpenziwe Joseph Boimanda katika sherehe itakayofanyika baadae mwezi huu siku ya mkesha wa X-mas.

Hivi karibuni, kitchen Party yake ilifanyika katika ukumbi wa Kassa ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Mwasiti ambaye pia ni afisa utawala wa Jahazi, ni mtoto wa aliyekuwa mwimbaji maarufu wa TOT Taarab, marehemu Leila Khatib.

Courtesy of Salut5.....
 



MOMBASA STARS KUIBUKA NA ALBUM MPYA MWAKA WA 2013.....

Bendi linalokuja kwa kasi sana mjini mombasa katika tasnia ya taarab yaani 'Mombasa Stars Modern Taarab' linajiandaa kuachia album mpya kwa jina la 'Nichombeze.'

Katika Mahojiano ya kipekee katika kipindi cha taarab kinachonoga kote mkoani pwani cha 'Kwa Raha Zangu kupitia Pwani FM, Sultan wa mirindimo Dr. Malik alipasua mbarika na kudokeza kuwa albamu hiyo itakuwa na vibao vinne ndani japo kwa sasa inaendelea kupikwa na itakamilika na kuzinduliwa mwaka wa 2013 panapo majaaliwa yake Mola.

Baadhi ya mistari katika kibao kitakachotambulisha album hiyo kwa jina la 'Nichombeze' kitakachoimbwa naye Dr. Malik ni,

"Nichombeze nichombezeke.... Mpaka vidughushi wakereke...Nnapenda raha zako zinanipa afya tele na pale nizikosapo hukonda kama unyelee....Nichombeleze kwa muala aaahh Niliwazeee miye....." 

Wakati huo huo, Dr. Malik aligusia hatma yake kwa sasa katika tasnia ya taarab na alisema,

"Mimi nipo katika muziki kama kawaida na nilitaka kuwatia tumbo joto kuwaangalia wale wapambe wasopenda tuwe katika sanaa lakini kutokana na upendo wa mashabik ndio kwa sasa tunaendelea na kazi ila sijajiondoa kama inavyosemekana," Akasema Dr. Malik.

Pia alididinda kuzungumzia kuhusu maisha yake ya kibinafsi ambapo inadaiwa kuwa ndoa yake ilikumbwa na msukosuko hivi karibuni hadi kupelekea kuachana na mkewe na kufikia sasa inadaiwa ameonekana akiwa na mpenzi mpya.

"Nisingependa kuyazungumzia hayo sababu sio muhimu ila ningependa tuzungumzie zaidi biashara wala sio maisha yangu binafsi," Akasema Dr. Malik. 

Haya yanajiri huku bendi hilo likishirikiana na lile la TOT likipanga kutambulisha album yao ya hivi karibuni ya 'Give us Time' kwenye tamasha la kufungwa mwaka litakaloandaliwa katika ukumbi wa Club Tropicana wakati wa mkesha wa mwaka mpya 2012/2013.

Tuesday 18 December 2012

ALBUM YA 'GIVE US TIME' KUZINDULIWA RASMI HUKO CLUB TROPICANA..........

Lisemwalo lipo na kama halipo lipo njiani laja na sasa ni RASMI kwamba macho yoteee mwaka huu yatashuhudia uzinduzi wa album ya kwanza ya taarab itakayounganisha mji wa Mombasa Kenya na Dar es salaam tanzania kwa mara ya kwanza katika tasnia ya taarab.

Katika mahojiano ya kipekee na blog hii/kipindi cha taarab cha 'Kwa Raha Zangu' kupitia Pwani FM, Sultwan wa Mirindimo Dr. Malik na Malkia wa Mipasho Bi. Khadija Kopa wamefichua kuwa album hiyo kwa jina la ‘Give us Time’ itatambulishwa rasmi tarehe 31 mwezi wa disemba mwaka huu wa 2012 katika ukumbi wa Club Tropicana.

“ Ni kweli tutazindua album hiyo usiku wa tarehe 31 mwezi disemba mwaka huu katika tamasha la kufunga mwaka katika ukumbi wa Club Tropicana hapa mjini Mombasa, kwa ushirikiano na bendi la TOT (Tanzania One Theatre) kutoka Tanzania, Mombasa Stars Modern Taarab na mabendi tofauti kutoka Kenya,” Akasema Bi. Khadija Kopa.

"Kwa sasa mipangilio ya kuandaa tamasha hilo linaloanza kuanzia saa tatu usiku hadi chee la ‘Pwani/Give us time Nyt’ yamekamilika na pia tutakuwa na surprise kadha wa kadha plus kiingilio ni shillingi 300/- tu kwahivo wajitahidi wapenzi wetu waje wajionee wenyewe, " Akasema Dr. Malik.

Wameahidi kuwapa wapenzi wao burudani la ‘high class’ likalalowapa raha mpaka barabarani.

“Yaani ni wakae mkao wa kula maana safari hii tutawaacha hoi kwa kuwapa burudani spesheli 
watakalolikumbuka daima na pia nakala za cd ya album hiyo zitapatikana kwa wingi siku hiyo kwahivo wajiandae kula raha,” Akasema Khadija Kopa. 

Album hiyo ya ‘Give us Time’ ina vibao vinne ikiwemo kibao kilichobeba album cha ‘Give us time’ kilichoimbwa na Dr. Malik akimshirikisha Khadija Kopa, Full Confidence by Dr. Malik, ‘Mjini Chuo Kikuu’ by Khadija Kopa na ‘Simtoi’ by Khadija Kopa.

Itakumbukwa kwamba fikra za kuunda album hii ya ‘Give us Time’ ilitoka baada ya wawili hao (Dr. Malik & Khadija Kopa) kuhojiwa kuhusiana na swala zima la kukuza sanaa ya burudani la taarab kanda ya afrika mashariki kupitia Pwani FM katika kipindi cha taarab kinachotikisa mkoa wote wa pwani cha ‘Kwa raha zangu.’

THABIT AIBUKA NA KIBAO KIPYA TEINAAAAAAAAAA.......

Hayawi hayawi mwishowe huwa, baada ya kuibuka na kibao kipya kwa jina la 'Hatuna Habari' ambapo alimshirikisha Mwanahawa Chipolopolo hivi karibuni sasa Mfalme wa kinanda Thabit Abdul ameibuka na kibao kingine kinachoitwa 'Habibi.'

Kupitia kibao hicho, Thabiti amewashikirikisha baadhi ya wasanii wa kundi la Mashauzi Classic kuleta fleva mpya katika tasnia ya taarab.


Mpiga kinanda huyo amekiimba kibao hicho kwa umahiri mkubwa, akimlalamikia kimwana, ambaye amekuwa akimtesa kimapenzi.


Juhudi za kumtafuta Thabit Abdul zinaendelea kwani amekuwa mteja hapatikani hivi karibuni na tutakapompata tutakupasha zaidi.

Wakati huo huo pia mwimbaji mkongwe wa fani hiyo, Ally Hemed Star vilevile naye hataki kushindwa na kuibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la 'Ni wewe.'

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Ally Star kuibuka na kibao cha taarab baada ya kuwa kimya kwa takriban miaka miwili

Kama ilivyo ada na desturi, utapata kuviskia vibao hivi kwa mara ya kwanza hivi karibuni kupitia Pwani FM...Tafrija Kipwani.

Additional Information Rusha Roho Blog...

Monday 17 December 2012

USWAZI USWAHILINI........HALOOOOOOOOO

Courtesy of  Henna Designs Arabic & Indian....

WAGOMBANO NDIO WAPATANO??????

Waambiwa ndugu wanapogombana shika jembe ukalime, wakipatana nenda ukavune... na kwa mara nyengine tena huenda mambo sio shwari kati ya mtu na nduguyee yaani Sauti ya Chiriku Bi. Khadija Yussuf na Big Daddy Mfalme Mzee Yussuf.

Akihojiwa kupitia kipindi cha ‘Sham Sham za Pwani’ kinachorushwa kupitia runinga ya ITV, Bi. Khadija Yussuf aliangua kilio akidai kuna ‘Vidudu watu’ ndani ya bendi la jahazi wanaopeleka maneno ya urongo kwa kaka yake ili kuwagombanisha kiasi cha kuwafanya wasielewane vizuri.

Alipoulizwa ni kitu kipi kinachomkera katika maisha yake.... Naye (Khadija Yussuf) bila kutafakari kwa muda mrefu alijibu kuwa, ni kile kitendo cha mtu kutoka aendako na kwenda kumzushia maneno ya uongo kwa Mzee.
 

"Kinachoniuma zaidi ni kwamba afadhali hayo maneno ningekuwa nimeyasema, lakini sijafanya hivyo, Hawa watu wanapaswa kutambua kwamba kuna Mungu na mimi na Mzee Yussuf tumezaliwa baba mmoja mama mmoja, atakapozikwa Mzee Yussuf ndipo nitakapozikwa mimi,"alisema Khadija huku machozi yakianza kumlengalenga.
 

"Kusema kweli maisha ninayoishi na Mzee Yussuf hivi sasa ni tofauti na huko nyuma tulikotoka, Inaniuma sana,"alisema Khadija na kuangua kilio kikali.
 
Mapema Khadija alisema kuna kikundi cha watu ndani ya Jahazi, ambacho kimekuwa kikimchonganisha yeye na wifi yake, Leila Rashid, ambaye ni mke wa pili wa Mzee.


Alisema watu hao wamekuwa wakipeleka maneno ya umbeya kwa Leila wakidai kuwa yeye ndiye ameyasema na vivyo hivyo wamekuwa wakija kwake na kumweleza maneno kama hayo.
 

"Kuna wakati Leila amekuwa akinitumia meseji zenye maneno machafu, Ninapomjibu anakasirika Sielewi tunachogombea ni kipi,"alisema Khadija.
 

"Binafsi sina tatizo na Leila na sioni kwa nini tugombane, Sielewi na ninashangaa, Lakini hii yote ni kwa sababu kuna watu ndani ya Jahazi wanaotuchonganisha kwa makusudi,"aliongeza.
 

Kwa sasa, Khadija alikariri kuwa anajiandaa kuibuka na kibao chake kipya kitakachojulikana kwa jina la 'Na bado. '

Alisema kibao hicho kitazinduliwa katika onyesho maalumu litakalofanyika Desemba 30/31 mwaka huu. 

Hata hivyo juhudi zetu za kumtafuta Mfalme Mzee Yussuf au mkewe Malkia Leila Rashid zinaendelea kwa sasa ili tubaini yanayoendelea kati ya watatu hao.

Hii sio mara ya kwanza kwa wawili hao (Mzee Yussuf na dadake Khadija Yussuf) kukosana kiasi cha kunyimana salamu na kusemana vibaya kwenye vyombo vya habari, hali iliyomplekea Bi. Khadija kulikacha kundi la Jahazi linalomilikiwa na Mzee, kisha kwenda kushiriki kuanzisha Five Stars Modern Taarab na akiwa huko, alidaiwa kumpiga madongo mengi kaka yake katika miaka ya hivi majuzi.

Haya yanajiri huku bendi la Jahazi chini ya uongozi wake Mfalme Mzee Yussuf likijiandaa kuzindua rasmi albamu yao mpya ya tisa kwa jina la ‘Wasiwasi wako ndio maradhi yako’ tarehe 30/31 mwezi huu katika mkesha wa mwaka mpya huko Travertine Hotel, Magomeni Dar es Salaam Tanzania.

Additional reporting Toto la Matashtiti Mwa4.../Rusha Roho Blog