Tuesday 5 March 2013

LEILA RASHID AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE......

Lujaina.
MKE wa Mzee Yussuf, Malkia Leila Rashid jana jioni alijifungua mtoto wa kike.

Leila alijifungua katika hospitali ya Dr Hameer iliyopo kariakoo na hali yake pamoja na mtoto ni nzuri.

Mzee Yussuf aliiambia Saluti5 (Mtandao wa burudani) kuwa Leila na mwanae wataendelea kuwepo hospitalini hapo kwa siku mbili tatu.

Kwa mujibu wa Mzee Yussuf, jina la mtoto (pichani) ni Lujaina.

 “Dua la mke wangu limepokelewa, alikuwa anaomba sana apate mtoto wa kike” alisema Mzee Yussuf.

Kwa hisani ya Saluti5.....The Screen Masters.


No comments:

Post a Comment