Tuesday 26 February 2013

LEILA RASHID KUJIFUNGUA HIVI KARIBUNI.....


MKE mkubwa wa Mzee Yusuf ambaye pia ni mwimbaji wa bendi la Jahazi Modern Taarab, Leila Rashid ‘’Malkia’’ anatarajia kujifungua muda wowote kuanzia sasa.

Kwa mujibu wa chanzo makini kilichoomba hifadhi ya jina lake, kwa kipindi kirefu Leila alikuwa haonekani kwenye bendi kutokana na ‘kuchoka’ na sasa ametimiza miezi tisa ambapo mumewe alimpumzisha kazini hadi atakapojifungua.

“Yah! Ni kweli mke wangu ni mjamzito na muda wowote kuanzia sasa anaweza kujifungua na baadaye atarejea kwenye bendi kama kawaida,” alisema Mzee Yusuf.

1 comment:

  1. namtakia kila la kheri ..Mngu atamjaalia salama in sha Allah

    ReplyDelete