Sunday 24 February 2013

OFFSIDE TRICK WAIBUKA NA NGOMA MPYA......

Wakali wa ngoma za mduara kule Dar es salaam Tanzania wameibuka na vibao vipya kadha wa kadha ikiwemo 'Usinipe' ambapo wamemshirikisha Baby J katika album ya Nipe Nikupe.

Waambiwa...'Nakifungua kifua nanena yalotimia ee
Kamwe sitogombania pale nilopotokea
Nakifungua kifua nanena yalotimia ee
Kamwe sitogombania pale nilopotokea

Sili kisicholika ingawa kitu jamali
Na vyema kimepikika na kurashiwa asali
Madamu ni cha shirika kula sitokubali
Kamwe sitohadaika kwa kibakuli cha wali
Kula kitu cha shirika hairidhi yangu hali

Usinipe kinyama kinukacho moshi
mila zetu sie ni sumu ndani ya upishi .....'


Haya yanajiri siku chache baada ya msanii wa mduara Ali Tall maarufu kama AT kutoka Dar es Salaam Tanzania kutambulisha vibao vyake viwili mwaka huu kwa jina la 'Hana Haya' na 'Asali.' 


1 comment: