Wednesday 16 January 2013

AT AIBUKA NA GOMA MPYA YA MDUARA 'HANA HAYA'.......

Mwimbaji wa Mduara na Kizazi kipya Ali Ramadhan 'AT' ameibuka na kibao chake kipya cha mduara mwaka huu wa 2013 kwa jina la 'Hana Haya.'

Safari hii AT alimshirikisha Bi. Salha Abdallah kutoka kundi la taarab la Dar es Salaam Modern Taarab katika kibao hicho.

Baadhi ya vipande katika kibao hicho ni kama.... "Wapi tena mwenzangu? Nenda kwa waziri wa umbeya na mambo yasiomhusu mheshimiwa hana haya...Makubwaaaa!!!...Yaliomshinda viumbo kunyang'anyua ukubwa kwa kugombea ubwabwa." 

Hivi sasa anajiandaa kukamilisha mkanda wa video yake na utaiona SOON......

Haya yanajiri huku kundi la 'Offside Trick' likimshirikisha Baby J likitarajiwa kuachia kibao chao kipya kwa jina la 'Usinipe' hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment