Sunday 27 January 2013

MASHAUZI CLASSIC WAANZA MAZOEZI YA NYIMBO MPYA.....

KUNDI kabambe la miondoko ya taarab, Mashauzi, Classic limeanza rasmi mazoezi makali ya kutengeneza nyimbo mpya.

Mmoja wa wakurugenzi wa kundi hilo, Thabit Abdul, ameiambia mtandao wa Saluti5 kuwa nyimbo hizo ni maandalizi ya albam yao ijayo.

Thabit amesema wanakuja kivingine huku akiahidi kuwa safari hii nyimbo zao zitaleta mapinduzi makubwa kwenye muziki wa taarab, kuanzia upigaji pamoja na mpangilio wa mashairi.

Mazoezi hayo yanaendelea katika ngome yao Kinondoni Hananasif, jijini Dar se Salaam. 

Kwa hisani ya Saluti5....The screen masters.


No comments:

Post a Comment