Wednesday 30 January 2013

MASHAUZI CLASSIC WAKAMILISHA NYIMBO ZAO MBILI MPYA.......


Thabit Abdul akiongoza mazoezi ya nyimbo mpya jana

Isha Mashauzi mazoezini jana

Aisha Othman Vuvuzela


Hashim Said "Mzee wa Majanga"

Jumanne Ulaya "J Four" akipiga gitaa la solo
 


Saida Mashauzi akiimba mazoezini jana

Mpiga kinanda Kalikiti moto Mafia

KUNDI la miondoko ya taarabu, Mashauzi Classic limekamilisha nyimbo mbili kati ya zitakazounda albam yao mpya ijayo.

Kuanzia wiki iliyopita, kundi hilo lilianza rasmi mazoezi ya kutengeneza nyimbo zao mpya na katika hali inayoonyesha uwezo mkubwa wa wasanii wao kukamata nyimbo tayari vibao viwili “Mimi mwanaume” na “Ropokeni yanayowahusu” vimekamilika.

Saluti5 ilitembelea mazoezi ya kundi hilo jana na kukuta nyimbo hizo zikiwa katika hatua za mwisho kabla hawajaanza kugusa nyimbo nyingine.

Wimbo “Mimi ni Mwanaume” umeimbwa na Hashim Said “Mzee wa Majanga” huku ule wa “Ropokeni yanayowahusu” ukiimbwa na Aisha Othman “Vuvuzela”. Nyimbo zote mbili ni utunzi wake Thabit Abdul.

Kwa hisani ya Saluti5....The screen masters.

1 comment: