Tuesday 1 January 2013

UZINDUZI ALBAMU YA ‘DOMO LA UDAKU’ HUKO DAR LIVE TANZANIA HAPO JANA..........

Mashabiki wa Dar Live wakiwa na furaha ya kuuona mwaka mpya na burudani ya taarab.
Umati ukirindima kwa burudani baada ya kutangaziwa kuwa mwaka mpya 2013 umeingia.
Kundi la Kings Modern Taarab likikonga nyoyo za mashabiki kabla ya kuwapisha T Moto.
Kundi la T Moto likizindua albam yake ya ‘Domo la Udaku’.
Mkurugenzi wa T Moto, Amini Salmini (kushoto) na muimbaji wa kundi hilo, Jokha Kassim (aliyevalia shela kama bi harusi) wakiingia jukwaani kimadaha.
Wapambe walioshika shela kwa nyuma wakinogesha hafla hiyo.
Jokha akikamua.
Wacheza kiduku nao wakimrusha roho ‘bi harusi’ kwa pembeni.
Uzinduzi wa albam ukiendelea.
Ni shangwe tupu ndani ya Dar Live.
‘Bi. Harusi’ akiondolewa jukwaani baada ya kumaliza kufanya makamuzi.
Muimbaji mpya wa T Moto aliyetokea Kings Modern Taarab, Ustaadh Issa Ally, akikamua.
UMATI mkubwa wa wasaka burudani ulifurika ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live huko Mbagala katika kusherehekea mwaka mpya ambapo pia kundi la taarabu la T Moto lilizindua albam ya ‘Domo la Udaku’

 (PICHA: RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY/ GPL).....Courtesy of Global Publishers

1 comment:

  1. hahahaha nimechokaje mie jamani Jokha kassim amefunika sio mchezo kavaa Veil..heee makubwa afu napenda alipobebwa na Amini Salmin..had rahaaaa

    ReplyDelete