Tuesday 1 January 2013

JAHAZI YAITIKISA DAR.......................

Mfalme Mzee Yussuf akizindua kibao chake 'Wasiwasi wako'
Umati wa mashabiki uliohudhuria uzinduzi wa Jahazi juzi
Waimbaji wa Jahazi wakiwa jukwaani tayari kwa uzinduzi
Hawa Hassan wa ITV  (kulia) A.K.A Toto la uhakika akiuliza swali maalum la kuzindua album
Mwanne Othman A.K.A Toto la Matashtit wa East Africa Radio naye hakuachwa nyuma
Mtangazaji wa Times FM, Ummy Suleiman ndani ya nyumba
Mohamed Mauji akikamua gitaa la solo
Mama kijacho, Malkia Leyla Rashid baada ya kumaliza kuimba wimbo wake mpya "Sitaki Shari"
MABINGWA wa mipasho, Jahazi Modern Taarab, usiku wa juzi walidhihirisha ubabe wao kwenye muziki baada ya kuzindua kwa kishindo albamu yao mpya, ‘Wasiwasi Wako’.

Uzinduzi huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Travertine Hotel, Magomeni, jijini Dar es Salaam, kuanzia majira ya saa 4 usiku  na kuendelea hadi usiku wa manane.

Huwezi kuamini, hadi saa 5 za usiku, tayari Jahazi walishavunja rekodi ya mahudhurio ya makundi mengine yote yaliyowahi kuzindua kwenye ukumbi huo.

Kiingilio cha sh. 20,000 hakikuwa kikwazo cha kuwazuia mashabiki pamoja na wapenzi kumiminika ukumbini humo na kujaa hadi kooni.

Kama ilivyotangazwa hapo awali, Jahazi walizindua albam yao bila kusindikizwa na msanii au kundi lolote lile.

Mzee Yussuf ambaye juzi aliingia jukwaani bila mbwembwe zozote, aliwaachia wapenzi fumbo moja: Aliuliza kama kuni inapikiwa, mwiko unafanyaje?

Na hayo yakijiri.....

Mzee Yussuf akiwa hospitalini jana jioni
MASAA machache kabla ya uzinduzi wa albam mpya ya Jahazi Modern Taarab, mkurugenzi wa kundi hilo, Mzee Yussuf alilazwa kwa muda hospitalini kufuatia malaria kali ilyompiga kwa takriban siku nne.

Mzee Yussuf alilazwa hospital ya Mico Kinondoni ambako kwa siku zote hizo nne alikuwa akienda hospitalini hapo na kulazwa muda wote wa mchana na kisha jioni anaruhusiwa kwenda kulala nyumbani kwake.

Hali hiyo ya ugonjwa, ilimfanya Mzee Yussuf atumbuize kwa shida jana usiku na mara baada ya kumaliza kuimba wimbo wake ilibidi akapate mapumziko mafupi.

Version yangu inakuja mda usiokuwa mrefu ila hii ni kwa hisani ya Saluti5 wa ukweee-eeh mtandao wa uhakika.


No comments:

Post a Comment