Sunday 23 December 2012

GUSAGUSA MINIBAND KUZINDUA 'UNAJIDODO LINAKUCHUKUCHA' MWAKA WA 2013.....

 
Bendi la Gusagusa Miniband linapanga kuzindua rasmi album yao ya kwanza kwa jina la 'Unajidodo Linakuchukucha' mwaka huu wa 2013 baada ya kukamilisha album hiyo.

Kulingana na mmoja wa wawakilishi wa kundi hilo Foni Chupaa, Album hiyo itazinduliwa rasmi mwezi ujao (Februari) na itakuwa na jumla ya vibao vinne ndani ikiwemo kibao cha 'Unajidodo linakuchukucha by Afua Suleiman, Mapenzi hayana Formula by Swabaha Salum, Usishindane na alojaaliwa by Maryam Alawy na Azurure atachoka/Inawaumaje by Ally Hassan.

"Tumeona uzinduzi kila mtu anazindua, tarehe yetu tumesogeza mbele kwa maoni na washabiki wa gsgs, na utakuwa uzinduzi babu kubwa kwa mara ya kwanza kwa hiyo matarajio yetu mwezi wa pili, lakini tutawatangazia rasmi tarehe ngapi na siku gani, na siku hiyo albam ya unajidodo itauzwa na kuanza kuwa maduka rasm." Anasema Foni Chupaa.

No comments:

Post a Comment