Friday 18 January 2013

LAMANIA SHAABAN: ‘MBUYU’ WA TAARAB ULIOACHA SIMANZI.....

HAKUWA mtu wa makuu na inawezekana wengi wakawa hawafamu uwezo wake wala sura yake …hakupenda kujikweza, lakini ni mtu mkubwa sana kwenye muziki wa taarab pengine kuliko yeyote unayemdhania wewe.
Marehemu Lamania Shaaban

Huyo ndie Lamania Shaaban aliyezikwa jana Tandika, Dar es Salaam huku akisindikizwa na mamia ya wasanii, wadau, ndugu, jamaa na marafiki waliopambwa na nyuso za huzuni.


Mwili wa Lamania aliyefariki juzi alfajiri ulipumzishwa katika nyumba yake ya milele majira ya saa saba za mchana.

Safari ya makaburini
Mwili wa Lamania Shaaban ukiingizwa kaburini
Mzee Yussuf ni kama haamini
 
Lamania aliyezaliwa mwaka 1969, mwenyeji wa Zanzibar, alikuwa ndiye mkurugenzi wa muziki wa East African Melody huku akiitungia zaidi ya nyimbo 40 ikiwa ni pamoja na kupanga mashairi na kutia sauti.


Lakini pia hata nyimbo zilizotungwa na watu wengine bado zilipita kwenye dawati lake na kuzifanyia uhariri. Alikuwa hana mpinzani katika gitaa la solo ndani ya Melody.


Alijiunga na East African Melody mwaka 1994 na kuanzia hapo akawa ni moja ya mihimili mikubwa ndani ya kundi hilo.
Mkurugenzi mkuu wa East African Melody, Hajj Mohamed akihojiwa na Hawa Hassan wa ITV
Watoto wa  Lamania Shaaban kutoka kushoto: Fatma, Mohamed, Nasria, Nasra na wa nyuma ni Shaaban

Wasanii kama Mzee Yussuf, Hajj Mohamed, Khadija Kopa, Bi Mwanahawa Ali, Hassan Soud, wote kwa nyakati tofauti waliiambia Saluti5 jana msibani kuwa Lamania ni pengo kubwa katika muziki wa taarab ambalo litachukua muda mrefu kuzibika. 

Huku hayo yakijiri....MWIMBAJI wa taraab wa Kings Modern Taarab, Hanifa Maulid, amsema licha ya kuvuna elimu ya uimbaji lakini pia marehemu Lamania Shaaban amemwachia kumbu kumbu kubwa.
 
Akiongea na Saluti5 jana, Hanifa alisema alibahatika kuishi maisha ya ndoa na Lamania ikiwa ni pamoja na kuzaa nae mtoto mmoja wa kike.

Enzi hizo marehemu Lamania na Hanifa Maulid
Hanifa Maulid akiwa na mtoto wake Nasra Lamania

Amesema japo baadae aliachana na Lamania, lakini mtoto huyo Nasra Lamania ndiye kumbukumbu pekee aliyoachiwa na mume wake huyo wa zamani.


Nasra anayesoma darasa la kwanza anaungana na watoto wengine wanne wa Lamania kutoka kwa mama mwingine kuunda jumla ya watoto watano waliachwa na marehemu. 
 
Kwa hisani ya saluti5...The screen masters.

No comments:

Post a Comment